Kwa mujibu wa shirika la habari la ABNA, likinukuu shirika la habari la Anatolia, huku Ufaransa ikijiandaa kutambua nchi ya Palestina, bendera za Palestina zimepeperushwa katika halmashauri 21 za nchi hiyo.
Kulingana na ripoti zilizochapishwa katika vyombo vya habari vya Ufaransa, inatarajiwa kwamba ndani ya masaa machache ijayo, nchi hiyo itatangaza uamuzi wake wa kutambua nchi ya Palestina katika mkutano wa kimataifa wa kiwango cha juu chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa kuhusu utatuzi wa suala la Palestina na utekelezaji wa suluhisho la nchi mbili.
Licha ya marufuku ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ufaransa, katika halmashauri 21 ikiwemo Nantes, Stains na Saint-Denis, bendera ya Palestina iliwekwa juu ya majengo.
Your Comment